To unleash the progressive power of a generation of Africans to reach beyond themselves and change the face of the continent forever. This is our time!

  • This is africamotivation.blogspot.com

    Watu wengi sana wamepotezwa mwelekeo wa maisha yao kwa sababu ya kushindwa kabisa kusema hapana kila inapobidi.Hiin ndio maana watu wengi sana wamepoteza muda wao kwa mambo ambayo hayachangii kabisa katika maisha yao na katika malengo yao by mr motivation - africamotivation.blogspot.com

  • This is africamotivation.blogspot.com

    Ni lazima uwe mtu ambaye una ujasiri wa kukataa mambo amabyo hayana msaaada katika malengo yako makubwa by mr motivation - africamotivation.blogspot.com

  • This is africamotivation.blogspot.com

    Muda waklo wa kuishi duniani ukipotea basi ujue hauwezi kabisa kuurudisha tena,hivyo ni lazima uamue kuutumia kufanya mambo ya msingi tu mr motivation by - africamotivation.blogspot.com

  • This is africamotivation.blogspot.com

    uwe mtu mwenye ujasiri wa kusema HAPANA kwa kila kitu ambacho unaona kinakuondolea mweleko uliioukusudia katika maisha yako by mr motivation - africamotivation.blogspot.com

  • This is africamotivation.blogspot.com

    Dont be shy and sad to let them go, if they are nothing to you dont hesitate by mr motivation - africamotivation.blogspot.com

To unleash the progressive power of a generation of Africans to reach beyond themselves and change the face of the continent forever. This is our time!
Share:

Audio>>pupa vs njia panda

Share:

Audio>>safari mafanikio

Share:

Audio>>Utafiti

Share:

» MJUE KIJANA ALIYEANZA KUMILIKI KAMPUNI AKIWA NA MIAKA 16,msome hapa kumjua na ujifunze mengi zaidi.

Kuna kijana anaitwa odense miaka 22
kutoka nchini Uganda anaeitwa Andrew
Mapuya.
Andrew anatokea katika famili ya chini sana
ambapo mwaka 2008 wazazi wake woote
walisimamishwa kazi.Jambo ambalo
lilipelekea nyumbani maisha kuwa
magumu.Wakati huo akiwa na miaka 16 na ni
mwanafunzi wa sekondari ikawa inamlazimu
aokote chupa za plastic auze na anunue
chakula cha nyumbani kwao.
Mwaka huo huo serikali ya Uganda ilipiga
marufuku matumizi ya mifuko ya plastic kwa
sababu za kimazingira pamoja na kiafya.Bila
kupoteza muda Andrew akatambua fursa kuwa
iwapo hakutauzwa mifuko ya plastic bado
mifuko itahitajika je mbadala wake ni nini?
Akawaza aanzishe biashara ya kutengeneza
mifuko ya karatasi yaani paper bag.Akafanya
ufatiti wa uhitaji wake wa mtaji ikawa ni tsh
za
uganda 36,000.Basi akaanza mdogo mdogo
kukusanya chupa za plastic anauza hela
anatunza ili kupata mtaji.Akatunza pesa
mpaka
alipobakiwa na kiasi kidogo kama tsh 11,000
akaenda kumuomba mwalimu shule
akampatia.Mwaka huo huo akasajili kampuni
yake ambayo inasemekana ndio kampuni ya
kwanza kusajiliwa ya kutengeneza na kuuza
mifuko ya karatasi.Kampuni inaitwa Youth
Enterprenual Link Investment (YELI)
Kampuni hiyo sasa inawateja wengi na
inatengeneza na kusambaza mifuko kwenye
super markets,restaurant,medical
centre,maduka,na makampuni mbali mbali
katika mji wa Kampala.Mpaka sasa
ameshaajiri
vijana zaidi ya 16.
Mwaka 2012 alikuwa mshindi wa shindano la
Anzisha Prize la vijana wajasiriamali na
alishinda dola za kimarekani 30,000
Ninachoweza kuona kama funzo kutoka kwa
kijana huyu ni kuwa
1.Unapotaka kuanzisha biashara fanya utafiti
2.Fanya biashara kwa kuangalia uhitaji wa
bidhaa husika yaani jamii inapungukiwa kitu
hicho
3.Kunapokuwa na shida ya kitu flani sehemu
flani hiyo ni Fursa ina maana unatakiwa
kuanzisha baiashara ili utoe suluhisho,ili utoe
huduma na automatical ndio biashara sasa
maana ina wateja.
4.Kwa vijana usisubiri mpaka uwe mtu mzima
ndio uanzishe biashara.Anzakuwaza mafanikio
sasa,anza kupanua mawazo yako na uchukue
hatua
Asante kwa kutembelea blog yako ya africa motivation
*@mr motivation*
Share:

JE, NINI CHA KUFANYA USIPOONA MATUNDA YA KAZI UIFANYAYO

Unakumbuka wakati unaanza kazi, kuna vitu
ambavyo ulitamani sana kuwa navyo,
ulitamani kuwa na chumba chako, angalau
chumba na sebule, kitanda, TV, kajiko ka gesi,
na vikorokocho vya ndani. Hembu angalia vile
vitu kama unavyo au huna na ulivipataje,
jiulize baada ya kuvipata pesa ya mshahara
uliyotumia kununua vile vitu iko wapi kama
sasa hivi huvinunui tena? Unajua ni kwanini
ulivipata hivyo vitu?
Huna haja ya kuumiza kichwa sana, ulivipata
kwakuwa ulikuwa na malengo na mtu
anapokuwa na mlengo flani basi moja kwa
moja huilazimisha akili yake kufanyakazi
kuelekea yale malengo. Kuna namna mbili za
kuweka malengo, namna ya kwanza ni kuweka
malengo bila kujijua “Unconscious Goals” aina
ya pili ni kuweka malengo ukiwa unajijua
“Conscious Goals”.
Aina hii ya kwanza ni ile ambayo kuna vitu
unapanga kuvifanya lakini si kwa mpangilio
au hukai chini ukasema haya ni malengo
yangu. Kama ambavyo ulisema unatamani
kununu TV na ukanunua hayo ni malengo
ambayo ulijiwekea, aina ya pili ni ile ambayo
unakaa chini na kuandika au kusema kabisa
mwaka huu nataka kufanya kitu A, B, Cna D.
Katika maisha mafanikio au vitu havidondoki
tu kama mvua ni lazima uviwaze na
kuviwekea malengo iwe ni kwa kujua kuwa
haya ni malengo au si malengo. Kwa watu
wengi ambao hawafanikiwa wanajikuta kuwa
badala ya kuweka malengo basi huweka
vikwazo. Kwamba kwa kuangalia mshahara
wako badala na kuuona mdogo badala ya
kuweka melango kutokana na mshahara wako
mdogo basi unajiweka vikwazo kutokana na
mshahara wako mdogo.
Hembu nifafanue kidogo, tuchukulia unapata
mshahara wa shilingi laki mbili kwa mwezi na
akiba ni shilingi elfu hamsini, kwa maana
kuwa hata ukijibana vipi utabakia na shilingi
elfu hamsini. Sasa umepata kiwanja cha
shilingi milioni moja, watu ambao
hawafanikiwi watawaza hivi “Mshahara wangu
mdogo siwezi kununua kiwanja cha milioni
moja”.
Lakini watu waliofanikiwa huweza hivi “Milioni
moja nikikusanya elfu hamsini hamsini, kwa
mwaka nitakuwa nalaki sita, hizi laki nne
zilizobaki kununua kiwanja ...ngoja niangalie
ofisini…siwezi pata mtu wa kunikopesha
kweli…hapa nikipunguza kupanda Bajaji…vipi
nikiwa napika mwenyewe si nita save…na
nikiuza na ile deki ya CD ambayo siitumiii…si
zitafika kweli…kuna na lile dili ofisini ngoja
ni….”
Umeona tofauti ya watu hawa wawili, yule
wakwanza baada tu ya kuona kuwa elfu
hamsini haitoshi kununua kiwanja cha milioni
moja alikaa kimya akasahau na
kujisahaulisha tena kuhusu kiwanja. Tena
utamsikia akisema “Sitaki kujipa tamaa za
bure, haya maisha ni lazima uridhike na
unachopata…” Lakini wapili yeye ataumiza
kichwa mpaka kupata anachokitaka, hivyo
ndivyo unavyotakiwa usiangalie usicho nacho
bali namna ya kupata cha kuongezea.
Asante kwa kutembelea blog yako ya makinspire.blogspot.com. karibu tena kwa kujifunza mengi zaidi
*@Mr motivation*
Share:

Video>>One of The Most Inspiring Speeches

Share:

Video>>THE WINNING MENTALITY - Powerful Motivation 2017

Share:

Video>>Study Hard AND Study Smart!

Share:

Jack Ma's Life Advice Will Change Your Life (MUST WATCH)

Share:

STOP WASTING TIME - Motivational Video for Success & Studying

Share:

6 Minutes to Start Your Day Right!

Share:

» UJASILI,KUJIAMINI-PANDA MBEGU YA UJASIRI KWA WALIO CHINI YAKO, soma hapa ujifunze jinsi unavyoweza kupandikiza mbegu ya ujasili.

Naona ni
vema  kujifuza jinsi ya 
kuwa msaada kwa walioko chini yetu
katika kuwajengea ujasiri. Kama
nilivyogusia awali, wengi wetu hawana
ujasiri leo kwa jinsi mazingira ya makuzi
yao yalivyokuwa. Wapo walio wahi
kunyanyasika na kunyimwa fursa za
kusema kitu mbele ya watu wazima, wako
waliokuwa wanapingwa katika chochote
kile walichowahi kukiongea. Sio kupingwa
tu, nafahamu pia wako waliokuwa
wanapokea kipigo baada ya kujaribu kitu
na bahati mbaya wakakosea kidogo. Watoto
hawa walitendewa haya katika mazingira
ya mashuleni au hata manyumbani, hapa
namaanisha walifanyiwa haya na walimu
au hata wazazi au walezi wao pasipo kujua
kuwa walikuwa wanapanda mbegu ya kuua
ujasiri katika maisha mazima ya utu uzima
wa watoto hao.
Yamkini wewe ni mzazi, kila unaporudi
nyumbani unamwona motto wako
anabadilika, anaogopa kukaa nawewe au
kusema na wewe kitu chochote wakati hana
kosa lolote, usinyamaze kimya, labda kuna
mazingira anayoishi na kukuzwa akiwa
shuleni yanayo muharibu taratibu. Yamkini
pia wewe ni mwalimu na unamshangaa
mtoto fulani jinsi alivyo muoga,
anayejificha nyuma ya wenzake na
asiyejaribu chochote, katika hili hutakiwi
kunyamaza kimya, labda kuna maisha
motto huyu anayaishi na kukuzwa
nyumbani ambayo yanaharibu utu na
ujasiri wake.
Bahati mbaya athari za makuzi haya
hazionekani kwa dhahiri sana mtoto awapo
mdogo, bali yeye mwenyewe anapokuwa
mkubwa anajishangaa yuko tofauti na
wengine. Lile analolitamani kulifanya au
kuliongea anajikuta hawezi kwasababu
hana ujasiri hata chembe. Kila ndoto
aliyowahi kuwanayo awali inafifia taratibu
na mwisho ina kufa. Katika mazingira haya
wakulaumiwa ni wazazi, walezi au
wanaotoa makuzi mashuleni. Wito wangu
kwa sisi wote ambao tunazungukwa na
jamii ya watoto ni kwamba tujitahidi sana
kuthamini ilembegu ya ujasiri ambayo
watoto wanaotuzunguka wamezaliwa nayo.
Iwe ni watoto wetu au wawenzetu, sote
tunawajibika kukuza na kuendeleza chembe
ya ujasiri ambayo watoto hawa wanayo ili
waweze kuiona kesho yao yenye mafanikio
makubwa. Mimi nimepata nafasi maranyingi
sana ya kuzungumza na vijana wakubwa
au watu wazima wengi ambao wamekuja
kufahamu wakiwa watu wazima kuwa
chanzo cha wao kutokuwa na ujasiri ni
makuzi waliyopokea kwa wazazi wao. Watu
hawa wengi wao wameendeleza chuki
kubwa sana na wazazi wao kwavile
wamekuwa wakijitazama kama
waliodhulumiwa kitu muhimu sana
maishani. Wako walioweza kusamehe
ingawa kwamaumivu makubwa sana.
Badala ya kuwa wakala wa kuua ujasiri wa
walewadogo wanaotuzunguka tuwe
mawakala wazuri wa kukuza na kujenga
ujasiri wao.
Asante
Endelea kutembelea blog yako bila kuchoka
Fb page: africamotivation
Blog: africamotivation.blogspot.com
You tube  chanel: africamotivation
Share:

» MAMBO MAZURI MUDA MWINGINE HUPITISHWA KWENYE NJIA MBAYA,soma hapa kujifunza mengi na update hamasa



Hivi umewahi kumuona mdudu kiwavi, kiwavi
ni mdudu mwenye sura mbaya sana na
mwenye umbo baya sana, kwasababu
anapokuwa kwenye harakati za ukuaji
anakuwa kama mfano wa jongoo, lakini kitu
kimoja ambacho kinanishangaza kutoka
kwenye huyu mdudu ni kwamba ni yeye huyu
huyu ambae siku moja anakuja kuwa kipepeo,
najiuliza tu swali moja unadhani kwa kipindi
hajawa kipepeo angesema basi bora nife kama
ndo niko hivi,kipepeo angetokea?laa hasha
asingetokea, angesema mimi ndo nimeumbwa
hivi hivi na maisha yangu ndo haya haya
Mungu kanionea namatumaini leo
tusingeuona uzuri wa kipepeo.

Na maisha yetu ndivyo nalivyo muda
mwingine mambo mazuri huwa yanapita
kwenye matukio mabaya ambayo huenda
huyapendi, siku moja alikuepo jamaa mmoja
alikuwa amechoka kabisa kufanya kazi
ambayo anaifanya, huenda ni kama wewe
ulivyochoka kwenda kazini kwasababu
unaamka mapema sana, huyu bwana kila siku
akawa anamuomba Mungu apate kazi kubwa ,
nzuri na yenye mshahra zaidi ya ule ambao
alio nao kwasasa.lakini apate kazi
ambayoatakuwa na furaha, aliomba saana tu,
siku moja Mungu akajibu dua yake, alipewa
kazi na boss akachelewa kuiwasilisha
kampuni ikakosa tenda, basi kesho yake
alipofika kazini alikuta barua ya kufukuzwa
kazi.

Daaah jamaa alilia sana sana tu kwanini
amefukuzwa kazi, familia yake itaishije,
siunajua wafanyakazi huwa wakiwa kazini
wanakuwa wameridhika eee hawawazi hata
kufanyabiashara au mambo yanaweza
kuwaingizia kipato cha ziada kwa muda wa
ziada, basi alilia sana nakuanza kumlalamikia
Mungu kuwa amemuomba apate kazi sasa
ndo kafukuzwa kabisa.
Baada ya kuteseka kwa muda kidogo na
maisha kuwa magumu kwaajili ya kufukuzwa
kazi akapata muda wa kuwa anasoma
magazeti kupoteza mawazo, siku moja
akakuta gazeti kuna kampuni imeanzishwa
anatakiwa mfanyakazi mwenye sifa kama
zake, akaenda kufanya usaili akafanikiwa
kupata kazi, akapata cheo kama kile kile
alichoomba kwa Mungu, mshahara ule ule na
akawa free, sasa tujifunze kitu unadhani
aisingefukuzwa kazi angepata muda wa kukaa
kusoma gazeti na kupata habari iyo kiukweli
ingekuwa ngumu.
Rafiki usihuzunike unapokuwa kwenye wakati
mgumu, kwenye wakati ambao Mambo
hayaendi sawa, jua Mungu anakutafutia nafasi
iliyobora zaidi endelea kupambana hadi
kileweke, dhahabu ili ing'ae sharti ichomwe
moto, usikate tamaa usihuzunike siku moja
utakuja kuishi maisha yaliyo bora.
USIHUZUNIKE MDUDU KIWAVI, SIKU MOJA
UTAKUWA KIPEPEO

*@Mr motivation*
Share:

WATANZANIA NA TABIA YA KULALAMIKA NA KULAUMU, soma hapa kujifunza mengi na kuacha tabia ya kulaumu na kulalamika

Mbona unalalamika kila siku kwamba biashara yako ni ngumu? Kwani wewe ulianzisha biashara yako kwa lengo gani? Malalamiko kutoka kwa wajasiriamali imekuwa ni sehemu ya Maisha yao. Kila unapojaribu kuongea na wajasiriamali lazima usikie malalamiko mengi ikiwemo--
ukosefu wa mitaji ya kuendesha biashara.
Watu wanalalamika eti hawafikiriwi, hakuna anayewajali na hawasaidiwi! Yawezekana ni kweli, lakini kwa yeyote mwenye malalamiko na aketi chini na ajiulize hili; “Ndiyo hakuna anayenijali, hakuna anayenifikiria na hakuna anayenisaidia, kwahiyo…...”

Ukishajiuliza swali la “kwahiyo…” --bilashaka utaamua mojawapo kati ya haya:
ama ni kuacha kufanya biashara au kuendelea na biashara”. Endapo utaamua kuacha biashara kero na malalamiko yako yote vitakuwa vimeishia hapo na kimsingi utaweza kuendelea na maisha mengine.
Endapo utachagua kuendelea na biashara, maana yake ni kwamba matatizo unayolalamikia si makubwa kiasi cha kukuzuia kupata faida na pengine ndiyo maana umechagua kuendelea na biashara bila kujali matatizo na changamoto zilizopo.

Utamaduni wa kulalamika juu ya kazi tunazozifanya tumeurithi kutoka kwa watumishi hasa waajiriwa. Mfumo wa ajira duniani uko katika umbo la pembe tatu (piramidi). Ambapo unakuta mkubwa ni mmoja na chini yake kunakuwa na watu wengi kutegemea na ukubwa wa taasisi au kampuni husika iliyokuajiri. Mara nyingi watu walioko chini wakishindwa jambo lolote umsukumia yule aliyejuu ili afikiri na kutoa suruhisho kwaniaba ya wale wote anaowaongoza.

Kwa maana nyingine ni kwamba katika umbo hilo hapa juu, kuna mambo mengine huruhusiwi kuyafanya au kuyatolea maamuzi isipokuwa aliye juu yako. Pili, ukiwa mwajiriwa wa ngazi za chini kuna mambo ambayo yakikushinda unayapeleka kwa mkubwa wako kwaajili ya ufumbuzi zaidi.
Kwahiyo, chimbuko la tabia ya kulalamika ni utaratibu wa kutegemea maamuzi ya aliye juu yako. Kama anayepaswa kuamua jambo fulani, hafanyi hivyo kwa wakati au akafanya maamuzi vibaya basi utakuta waajiriwa walioko chini wanafanyakazi kwa kunung’unika muda wote, wanalalamika muda wote wanasema hovyo muda wote na hasa wakiwa maeneo ya nje ya ofisi zao.
Ikumbukwe kuwa, kinachowapa waajiriwa uhalali wa kulalamika ni ule mfumo au utaratibu wa ajira duniani ambao unatoa nafasi kwa mwajiriwa kuweza kupeleka malalamiko yake ngazi za juu endapo ataona kuna mambo ambayo hayaendi sawa.
Katika mfumo mzima wa ajira “MKUU” ni mtu wa mwisho na hatutarajii halalamike kwasababu hakuna mtu mwingine aliye juu yake ambaye anatakiwa kumpelekea malalamiko, ingawaje wengine ujikuta nao wakilalamika kwa watu wa chini yao. Wewe kama ni “Mkuu” kazi yako ni kuamua na kutenda basi!

*@Mr motivation*
Share:

GET LATEST MOTIVATION AND INSPIRATION UPDATES VIA EMAIL

Enter your name and e mail.

Popular africa motivation posts

Recent africa motivation posts